Header Ads

test

VITA VYA WASHAIRI

1)Washairi kulumbana,ni nani alianzisha ?
 Washairi kugombana,lini tutatamatisha 
 washairi kuchukyana,jambo hili linatisha
 Vya maneno vinachosha,vi vita vya washairi.


 2)Washairi kupambana,jambo lisifurahisha
 Washairi kuungana,itaja tufunganisha
 Washairi kushikana,yaweza tuunganisha
 Vya maneno vinachosha,vi vita vya washairi.


 3)Washairi ndugu moja,mungu katukutanisha
 Tushaikaneni pamoja,manenoya twangusha
 Na subiri tukingoja,kabla kujitamkisha
 Vya maneno vinachosha,vi vita vya washairi.


 4)Washairi kupendana,babu alitufundisha
 Washairi kuzozana,kuna mengi litafisha
 Upendo na kupendana,nuru kutaiwakisha
 Vya maneno vianachosha,vi vita vya washairi.

 5)Kujiona ni mabingwa,ndiyo sumu twajilisha
 Baraka zote zafungwa,kitungo nawajulisha
 Kama balaa lajengwa,na miba tunajivisha
 Vya maneno vinachosha,vi vita vya washairi.


 6)Tushikaneni mikono,bila kujitenganisha
 Tuviache vimaneno,vya weza tuchonganisha
 Na kuleta malumbano,kisha kutupiganisha 
Vya maneno vinachosha,vi vita vya washairi

 7)Hovyo hovyo semeana,jambo hili lakondesha
 Ni ya nini kupondana,ni maovu twaendesha 
Tupendaneni kwa sana,sanaa kunenepesha 
Vya maneno vinachosha.vi vita vya washairi
 8)Kushaanza kulogana,tuhuma twazifurusha 
Haya tena twatajana,zetu jina twaangusha
 Hivi twavyofurushana,sifa zetu twachachusha
 Vya maneno vinachosha,vi vita vya washairi

 SHAIRI -VITA VYA WASHAIRI
 MTUNZI-Idd Ninga wa Tengeru Arusha
 iddyallyninga@gmail.com 
+255624010160 

Maoni 2 :

  1. Ushairi lengo lake,
    si jamii ibomoke,
    ni kusudi ijengeke,
    hii Ninga rai yake,
    INA UJUMBE MWANANA.

    JibuFuta
  2. Ushairi lengo lake,
    si jamii ibomoke,
    ni kusudi ijengeke,
    hii Ninga rai yake,
    INA UJUMBE MWANANA.

    JibuFuta