Header Ads

test

Ushairi katika zama za utandawazi.


.                        
Huseyn Jafari Juma

USHAIRI NA MSHAIRI  KATIKA ZAMA ZA UTANDAWAZI

Tar 21/ 3 kila mwaka ni siku ya ushairi duniani. siku  hii imeanzishwa  na shirika la umoja wa mataifa  linakoshughulika na elimu, sayansi na utamaduni (UNESCO)  mwaka 1999 kwa lengo la kuhamasisha usomaji,  uchapishaji,  ufundishaji wa ushairi duniani kote 

Marekani na  Kanada wameichagua tar 15/10  kama siku Ya kuadhimisha kuzaliwa kwa mshairi  mkongwe wa kiroma Publius Vergilius Maro aliyezaliwa 15/10/70BC

Lakini siku hii ya ushairi kwa nchi kama uingereza husherehekewa alhamis ya kwanza ya mwezi wa 10 kila mwaka ambapo mwaka huu itakuwa  tar 4

Kwahiyo Uingereza,  marekani,  na kanada wamechagua mwezi wa kumi katika kusherehekea siku ya ushairi duniani 

HISTORIA FUPI YA USHAIRI

Wataalamu wengi wa fasihi wamekubaliana kuwa  ushairi ulianza kipindi ambacho binadamu alianza kutumia lugha 
Kwa maana kuwa  wanahistoria wanaamini kuwa binadamu alipitia hatua mbalimbali za ukuaji   
Kuanzia mnyama  mwenye kutumia miguu minne 
Mnyama anayetumia miguu  Miwili  
Mpaka kwenye hatua ya kutoka kwenye unyama na kuwa mwanadamu kamili  na katika hatua zote hizi a mwanadamu ilikuwa  ni mbinu za kukabiliana na mazingira yake 

Baada ya kuwa binadamu kamili ndipo alipovumba lugha  na hapo  ndio ikawa chanzo cha ushairi  

 Hapo awali ushairi  ulitumika katika shughuli mbali mbali za kijamii kama matambiko na shughuli za uzalishaji mali kama kilimo, uvuvi,  n.k  
Katika shughuli za  kiuchumi Mashairi yalitumika  kuhamasisha... Tamaduni hizi zipo hadi leo  kwa mfano kwenye jamii za wadigo na wasukuma

Kabla ya mwanadamu kupata maendeleo ya kisayansi na kitknolojia ushairi ulihifadhiwa kichwani pekee  na hiyo ndio ilikuwa njia ya kurithisha ushairi kutoka kizazi kimoja kwenda Kingine 

UMUHIMU WA USHAIRI DUNIANI 

Kwa miaka yote  ushairi umekuwa muhimu zaidi katika jamii zetu 

1) ushairi umekuza  na kuendeleza lugha nyingi duniani ikiwemo kiswahili

Kwa miaka mingi washairi wamekuwa na kazi kubwa ya kukuza na kuendeleza lugha  kupitia kazi zao 
Mbinu za kutunga maneno mapya,   kazi zao mufti  zimeweza kueneza lugha  na kukuza lugha 
Lugha ya kichina, kigiriki, kilatini, kiarabu  na kiswahili ni miongoni mwa mifano bora 

 2) Ushairi umeleta usawa na kuzikomboa jamii nyingi duniani 

Nchi nyingi zilizotawaliwa, zilitumia ushairi kama njia ya kueleza mawazo yao juu ya watawala,  na pia kuhamasisha watu kujua haki na wajibu wao 
Pia ushairi umehamasisha watu kupigania uhuru kwa nchi zao 

Kwa mfano Tanzania  walitumia mashairi ya kiswahili kufanya hivyo 

Lakini pia ushairi ulitumika kwenye harakati za mtu mweusi huko marekani

 3) Ushairi unaibua matatizo yanayoikumba jamii na kuyatolea suluhisho
Ushairi umekuwa ukiibua matatizo mbali mbali ya kijamii na kuyatolea masuluhisho.. Mfano uongozi mbaya,  maisha magumu,  mmomonyoko maadili  n. k 

4) ushairi ni burudani 

moja wapo ya lengo kuu la ushairi ni   kuiburudisha jamii  ...maaana hata asili yake ni kumtoa binadamu katika upweke na uchovu ndiko kulikoleta ushairi 
Zama zilizopita ushairi ulikuwa ndio burudani nzuri zaidi 

Wafalme wengi walikuwa na washairi wao wa kuwaburudisha  
Pia mtume Muhammad  ('s. a. w)  alikuwa akipenda mashairi na alikuwepo mtu wa kumghania mashairi

USHAIRI NA MSHAIRI  

Tumeona historia fupi ya ushairi,  tumeona  umuhimu wa ushairi katika jamii  lakini Katika sehemu hii tutaangazia namna gani ushairi unavyomfaidisha mshairi 

Tumeona wacheza mpira wakipata pesa nyingi kutokana na mpira na fani nyengine kadhalika 

Je mshairi  anafaidika na ushairi wake??  

Hili ndio swali kuu  na ndio msingi wa mada hii 

Kama nilivyosema hapo awali  kuwa zamani  washairi walikuwa wakiwaburudisha wafalme,  lakini pia washairi walikuwa wakighani mbele ya watu wakapata kitu cha kuendeleza familia zao. Kwa mfano mshairi wa zamani aliyejulikana kama Raphael  na shairi lake la  The Parnassus 

Baada ya maendeleo ya sayansi na teknolojia  maandishi yaligunduliwa  na hapo ndipo ushairi ukaingia katika hatua nyengine ya uhifadhi 

Mashairi yakaanza kuandikwa kwenye  vitabu 

Maendeleo haya yalimpa mwanya mwengine Mshairi  aweze kukusanya mashairi yake na kuandaa kitabu ambacho aliwauzia watu  na faida yake hutegemea na nakala alizouza 

Na pia faida hutegemea jamii iliyomzunguka mshairi  kama ni ya wanaopenda kusoma vitabu  basi atafaidika kama sio hivyo basi hakuna apatalo mwandishi kwa mfano mtu kama Aristotle  aliandika vitabu vya ushairi na pia kuzungumzia ushairi kwenye kitabu chake cha  Poetics 
Mshairi wa kichina pia alindika  The Shijing 

Kukosekana kwa faida katika fani hii imepoteza washairi wengi walio na vipaji  ni washairi wachache saana walioweza kujitosa katika fani  bila kujali faida 

Lakini leo napenda kumzungumzia mshairi wa kiswahili katika zama hizi za teknolojia

Tukumbuke kabla ya hati hizi za kiswahili tunazozitumia Leo hii, kiswahili kilikuwa kikitumia hati ya kiarabu 

Na baadae  ndipo waingereza walibadili hizi hati tunazotumia leo hii 

Na pia tukumbuke ushairi wa kiswahili umepitia mikono ya washairi maarufu  kama Mwengo Bin Athuman  1728-1840 aliyetunga utenzi wa kwanza wa kiswahili UTENZI WA TAMBUKA,  Muyaka Bin muyaka,  Shaban Robert,  n.k

Lakini hawa wote walikuwepo kipindi cha maandishi tu hivyo wakawa wamejikita katika kutoa vitabu pekee 

Maendeleo ya sayansi na teknolojia huiamisha jamii kutoka katika aina flani ya maisha kwenda  aina mpya ya maisha 

Ni hivyo hivyo kwenye  ushairi  kuwa baada ya kugunduliwa kwa maandishi washairi walianza kuaandaa  vitabu  na kuyahifadhi mashairi yao kwenye maandishi 

Tokea kipindi hiko uuzaji wa vitabu  ndio ilikuwa  njia kuu ya  ya kumpatia kipato mshairi  

Hadi leo hii bado uchapishaji wa vitabu ndio njia kuu ya kumpatia kipato mshairi 

Hali inayoleta changamoto kwa washairi wengi hasa  ukizingatia jamii  za waswahili si zenye kupenda  kusoma  vitabu

Lakini  Changamoto kuu walizonazo washairi wa kiswahili ni mbili 

1) kutokuwa wa bunifu 

Kitu chochote kinachokosa ubunifu huisha ladha mbele ya jamii  kwahiyo ushairi wa kiswahili umekosa  ladha mbele ya jamii hasa kutokana na washairi wenyewe  kukosa ubunifu juu  ya fani yao 

Ni ubunifu gani ninao  uzungumzia hapa 

Kwanza lugha , lugha ndio jambo  muhimu katika ushairi..  Ushairi ni sanaa inayotumia lugha ya mkato katika kuwasilisha mawazo ya mshairi mwenyewe sasa ikiwa washairi wanakosa ubunifu katika  lugha zao inakuwa  ngumu  kuivutia hadhira  husika ili waweze  kuipenda kazi  yako 

a)  uteuzi wa maneno 

b)  uwasilishaji wa mada 

c)  uchaguzi wa mada 

d)  lugha ya picha na mbinu nyengine za  kisanaa 

Kama mshairi  utafanikiwa katika vipengele hivyo vinne  basi bila shaka mashairi yako yatakubaliwa na jamii 

Na hatimae kuanza kufaidika na matunda ya ushairi

   2) washairi kuwa mbali na teknolojia

Kuchapisha vitabu  ni jambo muhimu  lakini  kama wanataka kufaidika na ushairi wao  ni lazima waendane na kasi  ya teknolojia iliyopo 

Kwa mfano  kwa sasa watu wengi wamehama katika  kusoma  vitabu  vya hard copy bali wanaenda kusoma  online 

Watu wengi  wapo instagram  na YouTube 

Hivyo inatakiwa washairi wawafuate huko huko  kwa ubunifu wa kazi zao 

Kwa mfano waanze kughani mashairi yao kisha waya weke kwenye  YouTube  kazi zikiwa nzuri  ni lazima watu watayaangalia tu  hivyo wanaweza kupata malipo kupitia YouTube  na pia  kujitangaza mbele ya jamii  

Kuandaa  Video fupi za mashairi  na kuzipeleka instagram   hii pia itasaidia kuwatangaza washairi  na kupata wafuasi wengi wa kazi zao 

Hivyo vitu viwili kama vitafanywa kwa ubunifu wa hali ya juu unaweza  kumsaidia mshairi  kwa kiasi  kikubwa  

Kupitia  kazi hizo  unaweza  ukapata matangazo ya bidhaa  kupitia  Kazi yako 
Pia kama shairi  lako  ni zuri  linaweza kuwa ni muito kwenye simu za watu  kwani ukumbuke si watu wote wanapenda kutumia nyimbo kama miito kwenye  simu zao hivyo washairi  wanapoweza kutunga kazi zao nzuri  zinazoendana na wakati kuna uwezekano Mkubwa wa kufanikiwa

Tunga mashairi yanayoendana na wakati 

Ya kiislamu,  kikristo,  ya kimapenzi,  ya kuchekesha,  kuhusia,  mapenzi ya mama, mapenzi ya mke kwa mume,  na mume kwa mke,  mashairi yanayoendana na wakati au yaliyotawala vichwa vya habari  mitandaoni 

Yote hayo yanaweza kukusaidia katika kukutangaza na kukupa faida  hata baadae  utakapo toa kitabu kinaweza kupata soko 

JE HAYO YATAWEZEKANAJE 

kuna mambo yanawezwa kufanywa na Mshairi peke yake kama kuanzisha chanel ya YouTube,  kuangazia instagram 

Lakini kwenye masuala ya kampuni  ni lazima vyama vya ushairi viwe imara na kuanzisha makongamano na kuwashirikisha makampuni makubwa kama makampuni ya mitandao,  vinywaji,  n.k  na kuwaelezea ni kwa namna gani mnaweza kushirikiana nao  katika kutangaza  biashara zao  kupitia fani za ushairi ila kabla ya kuanzisha  hayo makongamano wanatakiwa washairi wenyewe  watie bidii katika kujitangaza kwa kazi zao ziwe nzuri zaidi

Lakini pia kuna swala la kupeana  nafasi  kwamba  sio  kila mshairi  anaweza  kughani na sio kila mghani anaweza  kutunga  hivyo  mshairi  asieweza kughipatet anatakiwa atoe nafasi  kwa mtu Mahiri wa kughani ili Kazi yao ipat ubora unaostahiki

TUKIFANIKIWA JUU YA HILO TUNAWEZA KUPATA FAIDA YA USHAIRI. 

tutakuwa tumeifikia jamii kwa kiasi kikubwa 

Na pia itakuwa tunaongeza kipato kupitia  ushairi

Ahsanteni

NB:  naruhusu kukosolewa na maoni kwa hichi nilichokiandiaka

Andiko hili limeandaliwa na  Mwl. Hussein Jafary  Juma 
(kipanga mtoa) 
0713115683
Tar 21/3/2018
Mwanza - Tanzania




Hakuna maoni